Monday 9 December 2013

Miaka 52 ya UHURU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amewashauri watu wanaopanga kulipa kisasi pindi watakapopata madaraka kuachana na mawazo hayo.  Rais Kikwete ametoa ushauri huo wakati akitoa hotuba yake kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya uhuru wa Tanzania Bara, ambapo ameelezea mengi mazuri aliyoyafanya rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela na kuwataka viongozi wa Tanzania kuiga mfano wa maisha yake ikiwa ni pamoja na kusamehe na kusahau bila kulipa kisasi.  “Najua kuna wengine hapa wamepanga kulipa kisasi, wanasema nikipata watanikoma.” Amesema rais Kikwete na kuwataka waache yaliyopita yapite na kuendelea kuganga yajayo, “acheni kulipa kisasi.” Rais Kikwete amesisitiza.  Hotuba ya Rais Kikwete ilijikita zaidi katika maisha ya mzee Nelson Madiba Mandela, katika kuungana na Afrika Kusini kuomboleza kifo cha kiongozi huyo shupavu na kutoa mfano wa jinsi viongozi wa Afrika wanapaswa kuiga mfano wa uongozi.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako