Monday 23 December 2013

HAPA MMOJA ATAAMKIA MUHIMBILI NA MWINGINE SEGEREA."TIMBWILI"

Mama mkwe kamkuta jamaa sebuleni kapandisha hasira anadai ataua mtu.
*MAMKWE*: Mwanangu kwani kuna nini jamani?
*MJAMAA*: Leo namuua mwanao, mshenzi sana?
*MAMKWE*: Tulia jamani kimetokea nini?
*MJAMAA*: Mwanao mshenzi nilikuwa nimesafiri, nikamtumia meseji kuwa nakuja, hajajibu; eti bado leo nimefika nimemkuta na mwanaume kwenye kitanda chetu dharau gani hii, sikubali leo tunagawana majengo ya serikali, yeye anaenda kulala Muhimbili mi naenda kulala Segerea
*MAMKWE*: Subiri kwanza mwanangu hayuko hivyo lazima kuna maelezo fulani kuhusu hili ngoja nimuulize...mama mkwe akamfuata mwanawe na baada ya muda akarudi sebuleni
*MAMKWE*: Unaona, nilijua mimi lazima kuna sababu. Kumbe mwenzio hakupata ile meseji uliyomtumia.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako