Thursday 18 June 2009

"VIJIMAMBO NDANI YA NDOA"


SULUHISHO LA UKIMYA

Mume na mke wake walikuwa na malumbano nyumbani wakaamua kunyamaziana kama suluhisho(silent treatment)
Mara mume alihamaki na kugundua kuwa itabidi amuombe mke wake amuamshe mapema alifajiri saa 11 ili aweze kuwahi ndege kwa ajili ya safari zake za kibiashara.Ila kwakuwa hakutaka kuwa wa kwanza kuvunja ukimya na hivyo kupoteza msimamo, aliamua kuandika ujumbe katika kipande cha karatasi ukisema "TAFADHALI NAOMBA NIAMSHE SAA 11 ALFAJIRI" Akaiweka mahali alipojua itakuwa rahisi mkewe kuiona, kisha akalala.
Asubuhi yake aliamka akijikuta amechelewa maana ilikuwa ni saa 3asubuhi. Akiwa amekasirika sana akitaka kumfuata mkewe na kumfokea kwa kutokumuamsha alivyoomba, akahamaki kuona kipande cha karatasi karibu na kitanda chake kimeandikwa " NI SAA 11 ASUBUHI SASA, AMKA MUME WANGU"
Tunajifunza nini hapa?????????????????????????????

No comments:

Post a Comment

Maoni yako