Sunday 21 June 2009

LEO NI SIKU YA BABA DUNIANI ("FATHER'S DAY")

Leo tunapoadhimisha siku ya Baba Duniani ("Father's Day") , ni wakati mzuri wa kumshukuru Mungu kwa kutupatia Baba duniani. Tuna mengi ya kujivunia na kuwashukuru wazazi wetu au hata walezi wetu. Je, umekumbuka kumkarimu Baba leo?

Kwa upande wangu mie(Mwenye Blog) namshukuru Mungu pia kwa kumwita kwake Baba yetu tarehe 23/03/2009 ambaye leo tungejivunia kuwa nae katika Maadhimisho haya. Shukrani zetu tunazipeleka katika sala tukimwomba Mungu ampumzishe mahali pema, Amina

No comments:

Post a Comment

Maoni yako