Nawatakieni kheri ya mwaka mpya 2010 wadau waheshimika. Nawaombeeni ili mwaka huu tuuanze vyema na tuendelee kujitahidi katika kila jema tuwazalo kulitenda tupate mafanikio siku hadi siku.
Hongereni sana kwa kuuona mwaka mpya.
Friday, 1 January 2010
Saturday, 19 December 2009
Saturday, 19 September 2009
SAFARINI
Kumradhi wadau, nilipata safari ya ghafla kuelekea Kijijini kwa Bibi na Babu kuhani msiba wa Baba yangu mzazi, na mtandao huku hakuna kabisa. Muda mfupi ujao nitarudi na kuwaletea yaliyojiri.
Salaam kutoka Kijijini
Salaam kutoka Kijijini
Wednesday, 2 September 2009
Tuesday, 1 September 2009
KARIBU DAR ES SALAAM ZOO
Monday, 31 August 2009
MASANJA WA ORIJINO KOMEDI KWENYE BLOG
MWISHO WA MWEZI
Mwisho wa mwezi umewadia, tunapoganga yaliyopita,pengine picha hii inaweza kukukumbusha mengi. Zingatia kusamehe waliochukizwa na mafanikio yako, na jitahidi kuimarisha mafanikio uliyopata mwezi mzima,na yawe kichocheo cha mwezi ujao. Jitahidi kupunguza wakuchukiao kwa kuwa "mtu wa watu", na pengine kwa kuweka mipaka.
Nawatakieni nyote Mwisho mwema wa mwezi na mwanzo mwema wa wiki.
Nawatakieni nyote Mwisho mwema wa mwezi na mwanzo mwema wa wiki.
Sunday, 30 August 2009
WADAU NAWATAKIENI JUMAPILI NJEMA
Saturday, 29 August 2009
NOTI MPYA YA SHILINGI 2,000

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa noti mpya za Sh2,000 ambazo zitatumika sanjari na zilizopo kwenye mzunguko kwa sasa.
Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu alisema jana kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari kwamba, lengo la kutoa noti hizo mpya ni kukidhi mahitaji yake kwenye mzunguko wa fedha nchini.
"Noti hizi mpya zinatofauti moja tu na zile ambazo zimo kwenye mzunguko kwa sasa nayo ni saini zilizopo.
Saini zilizopo kwenye noti mpya ni za Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo na Gavana wa Benki kuu ya Tanzania,” alisema.
Profesa Ndulu alisema kuwa noti hizo bado zina rangi ya kahawia, zikiwa na michoro inayoonyesha mandhari ya kitanzania kiuchumi, kiutamaduni pamoja na urithi wetu na mazingira.
"Mbele ya noti, bado kuna picha inayoonyesha utajiri wetu wa kuwa na mojawapo ya wanyama pori wakubwa yaani simba ,alama ya kificho ya twiga ambayo bado ipo kama ilivyo katika noti nyingine zinazozunguka sasa" lilifafanua tangazo hilo.
Alama nyingine zilizopo katika noti hiyo ambazo hazina tofauti na iliyopo kwenye mzunguko ni nyuma ya noti kuna picha inayoonyesha picha ya ngome kongwe illiyopo Forodhani jijini Zanzibar.
Vile vile, alisema zina picha ya kinyago cha kuchonga na alama ya usalama inayobadilika rangi ikigeuzwa.
”Benki kuu inawashauri wananchi kuwa hakuna haja ya kubadili noti hizo kwani thamani yake ni ileile na kwamba haina mpango wa kuzifuta zilizokuwepo katika mzunguko wa awali.
Habari imeandikwa na Burhani Yakub wa gazeti la Mwananchi.
Subscribe to:
Posts (Atom)








