Ndege aina ya Boeing 777-200ER ya Shirika la Ndege la Malaysia inasadikiwa kuanguka kusini mwa bahari ya China. Ndege hiyo ilikuwa na abiria 227 na wafanyakazi wa ndege 12 ilikuwa ikitokea Kuala Lumpur kuelekea Beijing China. Masaa 2 baada ya kuruka, ndege hiyo haikuonekana katika vyombo vya kuongozea ndege. Mpaka sasa juhudi zinafanyika kujua ilipoangukia na hali za abiria. Hata hivyo vyombo vya habari vya nchi inayohusika vimewatahadharisha ndugu na jamaa kuwa wajiandae kupokea habari ambazo zinasadikiwa zitakuwa si njema.
BASATA Yashukuru DCEA kwa Kurejesha Afya ya Chid Benz
34 minutes ago
No comments:
Post a Comment
Maoni yako