Wednesday 12 March 2014

KIJANA MREFU WA KITANZANIA ZAIDI YA HASHEEM THABEET

Huyu ni Baraka kijana mrefu kitanzania

Inasemekana ni kijana mrefu kuliko wote Tanzania. Kijana huyu (katikati pichani) ambaye anadhaniwa ni mrefu kuliko vijana wote Tanzania anaishi maeneo ya Gongolamboto, Banana jijini Dar es salaam. Kijana huyu huwa haonekani sana mitaani, lakini aliingia mjini siku hiyo na kuleta kizaa zaa kikubwa pale alipoibuka mitaa ya Aggrey, Kariakoo. Alikuwa kivutio kwa kila aliyemuona, alifunga mtaa watu wakimshangaa na kumgombania kupiga nae picha. Kila aliyetaka kupiga nae picha alitoa Shilingi elfu moja Tsh. 1000.
Picha hiyo amepigwa ndani ya Kinyozi (Salon) aliyoingia kupunguza nywele zake na umati wa watu walikuwa nje ya kinyozi huyo kumsubiri atoke. Mpaka sasa hajajulikana jina lake kamili na anafanya nini. Inasemekana kuna watu wanamfuatilia kumsaidia umaarufu.(Kwa hisani za Xdeejayy blog)
Hapa ni Baraka alipokutana na Hasheem

No comments:

Post a Comment

Maoni yako