Thursday 8 September 2016

"SINA MPANGO WA KUHAMA CHAMA"-PROFESA LIPUMBA

Profesa Ibrahim Lipumba aliyekuwa mwenyekiti wa CUF, amesema hana mpango wa kuhamia chama chochote pia hana mpango wa kuanzisha chama chake.
Profesa Lipumba amesema hayo katika kipindi cha Powerbreakfast kinachorushwa na Clouds FM alipokuwa akielezea msimamo wake juu ya CUF.
Katika mahojiano hayo Profesa Lipumba amesema Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif alikosea kumnyima mkono Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kwa kuwa unapokwenda kwenye msiba jambo la msiba lilipaswa kutawala.
“Hata mimi nilipokutana na Maalim baada ya kunikatalia kurudi kwenye uenyekiti tulisalimiana.”

No comments:

Post a Comment

Maoni yako