Tuesday 27 September 2016

NDEGE YA PILIYA "AIR TANZANIA" ILONUNULIWA CANADA YAWASILI LEO

KWANINI TUMENUNUA BOMBARDIER?

Shirika letu la ndege lilikufa kwasababu ya kushindwa kujiendesha kutokana na gharama kubwa za uendeshaji pamoja na ufinyu wa abiria wanaotumia usafiri wa anga!

Mwanzo nilifikiri labda ni wizi unafanyika lakini baada ya kujua gharama chache za uendeshaji nikaona ni sawa kwa shirika hili kushindwa kujiendesha.

Naomba nianze na bei ya Boeing

Boeing inauzwa dola milioni mia mbili tisini na sita(US296millions) wakati Bombardier Q400 inauzwa dola milioni 35 tu(US35millions)

Kumbe badala ya kununua Boeing moja ni heri tuongezee dola milioni kumi na tisa(US19millions) tununue Bombardier tisa(Bombardier 9)

Hesabu yake:

Boeing price US296 millions
Bombardier Price US35 millions
(35×9=315)
315-296=19

Ambapo hizi Bombardier tisa zingetusaidia kwa upande wa shirika kujiendesha lenyewe na kutupatia faida kubwa kwa mara tisa kwa Taifa.

Kuhusu Speed ya Boeing ni kweli ni kubwa kuliko Bombardier kutokana na uchomaji wa mafuta, Speed yake ni 590mph wakati speed ya Bombardier ni 414mph au 667km/h

Kama kutoka Dar to Mwanza ni Km 1100 maana yake Bombardier itatumia saa moja na dakika arobaini (1 hr and 40mnts) wakati Boeing itatumia saa moja na dakika kumi na tano(1hr and 15 mnts) tofauti ni dakika 25 tu

Boeing inatumia dumu moja la mafuta la lita 4 kwa sekunde moja kwa hiyo kwa lisaa limoja inatumia lita elfu kumi na nne mia nne (14,400) (4l×60s×60m)

Kwa mfano:

Mafuta ya ndege kwa lita yakiuzwa shilingi 2000 maana yake ili tutie mafuta ya kuelekea safari ya Songea inayochukua takriban saa moja tu tunahitaji milioni 28,800,000(14,400×2000)
Na tunahitaji abiria 96 watakaolipa Tsh 300,000 ili kuweza kulipia gharama za mafuta tu.

Hapo hatujajumlisha gharama za service na wafanyakazi na wala hatujapata faida yoyote

Bombardier inatumia 1.187lita ya madumu ya mafuta kwa mile moja yaani ukikadiria inatumia lita moja ya mafuta kwa mile moja (1mile=1.6kms)
Songea to Dar Air Distance ni takribani kilometa 537=335.625miles

Kwahiyo itatumia lita 398.386875 ambazo ukizizidisha kwa gharama ya Tsh 2000 kwa lita unapata laki saba tisini na sita elfu mia saba sabini na tatu=796,773

Kiuchumi kugharamika 28,800,000 na kugharamika 797,000 bora kipi?

Kwa mtu yeyote mwenye akili timamu na mwenye kutaka shirika hili kujiendesha kwa kibiashara ni lazima atumie Bombardier ili apate faida.

Pia kutokana na hali ya viwanja vyetu ndege hizi zinafaa kwa sababu zinaweza kutua katika viwanja vya kawaida ndio maana serikali ilizinunua ndege hizi mahususi kwa safari za ndani!

Hizi ndege Bombardier Q400 zinatumika Marekani na wanaendelea kununua Shirika la ndege la American Eagle wanazo Bombardier 35 Uingereza nao shirika la ndege la Flybe wamenunua 40.

Australian Air wamenunua 20
Ethiopia wamenunua 4 kufikisha idadi ya Bombardier 19.

Hatuwezi kutenga bajeti ya serikali iende ikahudumie shirika la ndege ambalo ukitumia akili ya kiuchumi hili shirika linaweza kujiendesha na likaliletea faida Taifa na kuliinua kiuchumi.

Hatupo kwa ajili ya kujishow off kutumia ndege za gharama kubwa na zisizo na faida ili watu watuone tuna ndege kubwa no!

Tupo kwa ajili ya kuliendeleza Taifa letu kwa faida liendelee mbele

No comments:

Post a Comment

Maoni yako