Wednesday 7 September 2016

HII NDIO "MBEGE"; ASILI YAKE KILIMANJARO

Mbege ni kinywaji asilia cha wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro. Ni kinywaji chenye kilevi na hivyo chatumiwa tu na watu wanaozidi umri wa miaka 18. Katika kunywa kinywaji hiki, wakazi hawa kiasilia hutumia kifaa kiitwacho "kata" ambacho kinatokana na kibuyu kama unavyoona kwenye picha hapa chini. Kinywaji hiki hutengenezwa kwa ndizi mbivu zinazopikwa kwa muda mrefu kisha kuachwa kupoa kidogo, kisha kuwekwa kwenye kifaa maalumu kiitwacho "kihondi" au siku hizi hutumia pipa kubwa. Baadae huwekwa ulezi uliosagwa na kuachwa kwa siku kadhaa, kisha ukamuliwa-huchugwa kwa vifaa maalumu na kuwekwa ulezi uliopikwa kidogo na kuandaliwa tena kitaalamu. kisha huwa tayari kwa kutumika.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako