Friday 3 June 2016

KATUNI YA LEO KUHUSU "WASANII FULANI"

Hivi karibuni gazeti moja la udaku liliwachora mastaa wa kike wenye uhusiano na mastaa wa Bongo wanaowazidi umri. Mastaa hao ni pamoja na Jacqueline Wolper aliyechorwa akimnywesha uji mpenzi wa Harmonize anayeonekana akiwa amebeba mdoli.

Wengine ni Wema Sepetu akiwa amempakata Idris Sultan, Zari the Bosslady akimweka Diamond kwenye kitolori cha kuwafundishia watoto kucheza na Aunty Ezekiel akiwa amembeba mgongoni mpenzi wake Mose Iyobo.

Ni Wema pekee ndiye aliyeijibu kwa kupost picha hiyo kwenye akaunti yake na kuandika: Aliechora hii natamani tu nimuone… Nimpe mkono.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako