Tuesday, 23 October 2012

HAPPY BIRTHDAY NICKY

Tumia kifaa hiki kutambua Birthday Party inafanyikia wapi? Hakuna kiingilio

Wadau, leo ni "bethdei" yangu. Napenda kuwashukuru nyote kwa fadhila za kila namna, furaha mlizonipatia hadi nikaweza kufikia siku ya leo. Mungu awakarimu sana na tuzidi kuombeana na kushirikishana fadhila. Karibuni soda tutakiane "Maisha Marefu"

Monday, 22 October 2012

JUA KALI, HALI TATA ZA MAISHA



Kila kukicha hali ya maisha inaboreka kwa baadhi ya watu na inazidi kuwa tata kwa baadhi ya watu. Wakati wengine wanajitahidi kuboresha maisha, wengine mchana wa jua kali wanapata kinywaji asilia. Lakini tujiulize, mapumziko haya yanayosindikizwa na kinywaji hiki yanatokana na kwamba watu walishafanya kazi muda wa asubuhi, na hivyo wanastahili kupumzika au????

Sunday, 21 October 2012

JUMAPILI NJEMA

Bado mapumziko ya wiki yanaendelea, nami niwatakie jumapili njema na mapumziko mema.

Saturday, 20 October 2012

ADHA YA USAFIRI SI BONGO TU

Baada ya pilikapilika za siku nzima kuboresha maisha kwa kazi, jioni inapofika ni kipindi cha kurudi nyumbani kupumzika, lakini unapofikiria adha hii ya usafiri, uchovu unazidi. Lakini kwa wakati huo huo, kwa wenzetu hali tata ya usafiri inafanya magari kujaza sana na hata bodaboda ichukue zaidi ya abiria 7.


ASUBUHI HIVI....JIONI HIVI....


Maisha ni mzunguko. Leo mambo yapo hivi, kesho yapo vile. Japo ni mwisho wa wiki, nawasihi wadau wenzangu tuendelee kupambana kufanya maisha yaende mbele na kwa mafanikio maana mwisho wa siku nguvu zinakuwa zimepungua sana na utendaji kazi unapungu. Picha hizi zikufikirishe. Weekend njema wadau.

Friday, 19 October 2012

KARIAKOO HALI SI SHWARI





Habari za hivi punde zinadai kuwa kuna hali mbaya katika maeneo ya Kariakoo jijini Dar e Salaam ambapo polisi wanapiga mabomu ya machozi kutawanya waislam wanaoandamana.
Kwa mujibu wa watu waliopo kwenye maeneo hayo maduka mengi yanafungwa na watu wanajifungia kwenye maduka hayo. Ingia hapa kwa taarifa zaidi:http://www.bongo5.com/breaking-kariakoo-pachafuka-mabomu-yanapigwa-kila-kona-10-2012/

KARIBUNI MLO WA MCHANA (LUNCH)

Wadau leo inabidi twende mpaka Bukoba ili lunch yetu inoge

NILIJUA UTACHEKA!


Jamaa watatu walikodi hoteli yenye gorofa 60, wao wakapata gorofa ya mwisho kabisa. Wakapanda kwa lifti na asubuhi wakashuka kwa lifti. Jioni waliporudi wakakuta umeme umekatika.
Wakakubaliana wapande ngazi kwa story. Wa kwanza akapiga story za kutisha kuanzia gorofa ya 1 mpaka ya 20, wapili akapiga strory za kuchekesha kuanzia gorofa ya 21-40 na watatu akandamiza story za kuhuzunisha kuanzia gorofa ya 41-60. Walipofika ya 59 yule watatu akasema hii ndio ya kuhuzunisha zaidi...TUMESAHAU KUCHUKUA FUNGUO PALE MAPOKEZI.

Hapa jamaa kaona kawin kweli kweli, kumbe hasara za kukumbia umande......soma kaka soma

ASUBUHI NJEMA

Labda tuanze siku yetu na kutafakari picha hii inayosisitiza kufungua macho. Watani wanasema, "kusoma hujui, hata picha nayo huioni"???

TUIGE LAKINI..........

Kwa sasa nchi yetu ya Tanzania ipo katika mchakato wa kupigia kura baadhi ya vivutio vilivyopo nchini(Serengeti, Ngorongoro, Mlima kilimanjaro, fukwe za zanzibar, mapango ya Amboni n.k.), ila walau kimojawapo kiingizwe katika orodha ya maajabu ya Dunia. Tuangalie na hiki kisijekuwa mojawapo ya maajabu.