Saturday 18 March 2017

MHE TUNDU LISSU, ACHAGULIWA KUWA RAIS MPYA WA TLS

Wajumbe wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), leo wamefanya uchaguzi wa kumchagua rais pamoja na wajumbe wa ngazi mbalimbali za uongozi wa chama chao.

Uchaguzi huo umefanyika mjini Arusha ambako wanachama wa TLS wamekutana kutekeleza ratiba hiyo pamoja na kupanga mipango mbalimbali ya utendaji kazi wa chama hicho.

Matokeo ni kama ifuatavyo:

Urais: Kura zilizopigwa 1682
Tundu Lissu 1411 sawa na asilimia 88
Francis Stolla 64
Victoria Mandari 176
Godwin Mwapongo 64
==>Kwa upande wa nafasi ya Makamu wa Rais (TLS) mshindi ni Godwin Ngwilimi aliyekuwa Mwanasheria wa Tanesco na kutimuliwa kwa kupinga Escrow.

Council Members
Jeremiah Motebesya
Gida Lambaji
Hussein Mtembwa
Aisha Sinda
Steven Axweso
David Shilatu
Daniel Bushele

No comments:

Post a Comment

Maoni yako