Friday 20 November 2015

WAZIRI MKUU MH.MAJALIWA KASSIM MAJALIWA AAPISHWA RASMI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli akimuapisha Kassim Majaliwa Kassim kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika hivi karibuni, hafla ya kiapo ilifanyika leo Ikulu ya Chamwino Mkoa wa Dodoma
Rais John Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa na mkewe Mary Majaliwa baada ya kumwapisha Waziri Mkuu kwenye ikulu ndogo ya Chamwinomjini Dodoma Novemba 20, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Mhe.Waziri Mkuu akipongezwa
Picha zaidi za tukio
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na mtoto Majaliwa mtoto wa Waziri Mkuu mpya kwenye viwanja vya Ikulu ndogo Chamwino wakati wa sherehe za kuapishwa Waziri Mkuu mpya wa awamu ya Tano, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa zilizofanyika leo Nov 20,2015 mjini Dodoma.
Waziri Mkuu mpya wa awamu ya Tano, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, akimpongezwa na mkewe baada ya kuapishwa rasmi leo kwenye Viwanja vya Ikulu ndogo Chamwino mjini Dodoma, leo Nov 20, 2015
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli (katikati)akiwa katika picha ya pamoja na familia ya Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa Kassim (watatu kushoto mstari wa nyuma) baada ya kuapishwa rasmi leo katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma,Picha na Ikulu.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako