Thursday 8 June 2017

BAJETI YA SERIKALI 2017/2018 YASOMWA LEO BUNGENI

Wakati Bajeti za Mwaka 2017/18 ikisomwa, tujikumbushe picha za Waziri wa Fedha miaka za 90 Luteni Kanali Jakaya Kikwete akisoma Bajeti
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango ametangaza kufutwa rasmi kwa ada ya mwaka ya leseni ya magari. Amesema uamuzi umechukuliwa ili ada hii ilipwe mara moja pale gari linaposajiliwa na baada ya hapo iendelee kulipwa katika ushuru wa bidhaa katika mafuta ya petroli na dizeli. Hayo yameelezwa leo Alhamisi bungeni na Waziri Mpango wakati akiwasilisha bajeti ya mwaka 2017/18.
Serikali imetangaza kufuta ushuru wa huduma kwenye nyumba za kulala wageni. Hayo yameelezwa leo (Alhamisi) bungeni na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Phillip Mpango wakati akiwasilisha bajeti kuu ya mwaka 2017/18. Pamoja na ushuru huo, pia Serikali imefuta ushuru wa mabango yanayoelekeza mahali zinapopatikana huduma za kijamii kama vile shule na hospitali.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako