Tuesday, 5 March 2013
DANGANYA TOTO
Wakati bado tunajiuliza kulikoni kuhusu matokeo mabaya ya Kidato cha nne 2012, hili nalo ni la kutupia macho, lisibaki kichekesho tu
UJUMBE WA LEO
Katika harakati hizi za kujikwamua kimaisha, ujumbe huu watukumbusha jambo fulani. Si vibaya kwa wale walioguswa kuzingatia undani wa ujumbe huu. Tafadhali usiusome ujumbe huu kwa papara na kukimbilia kulalamika au kukosoa.
MOTO-LEO
Moto umetokea tena leo na kuunguza baadhi ya ghala katika eneo la Uwekezaji la Shekilango Jijini DAR. Bado haijajulikana vizuri moto huo ulianzia wapi, ila mpaka picha hii inapigwa bado moto huo ulikuwa haujaweza kuzimwa kutokana na moshi mweusi kutanda juu ya eneo hilo na kusababisha usumbufu wa wahusika wa zima moto. Ikumbukwe kuwa moto huu unatokea baada ya tukio kama hili kutokea huko Mbezi- Kiwanda cha Chemi and Cotex, Mwenge madukani kwenye kituo cha Daladala na juzi tu huko Tegeta.
INATIA HURUMA
Wakati kila mmoja anajaribu kupambana kutafuta unafuu wa maisha, tunapaswa kwa wakati huo kuangalia wale ambao bado hawajiwezi kujitafutia wenyewe kama watoto hawa. nani anasikia kilio chao. Kilio hiki kinatokana na mambo mengi ya kimaisha, pengine ni ukosefu wa lishe, makazi, vita, ugomvi baina ya wazazi na mengine kama hayo. Ni wakati ambapo Serikali na watu husika waangalie hili maana inatia huruma.
Monday, 4 March 2013
Friday, 1 March 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)












