Friday 31 July 2015

BARABARA KIA - MERERANI KUJEGWA KWA KIWANGO CHA LAMI

Baada ya kilio cha muda mrefu kuomba wajengewe barabara ya Kia-Mererani kwa kiwango cha Lami, Serikali kupitia Waziri wa Ujenzi Mhe. John Magufuli amekamilisha maandalizi na hivyo ujenzi kuzinduliwa rasmi leo. Barabara hii ni muhimu itokayo Kiwanja cha Kimataifa cha ndege cha Kilimanjaro,kwenda yapatikanapo madini ya TANZANITE.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Pombe Magufuli, na baadhi ya viongozi wakifunua kitambaa kwa pamoja kuashiria kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Kia-Mererani, wakati wa hafla fupi iliyofanyika mji mdogo wa Mererani, leo Julai 30, 2015.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi

No comments:

Post a Comment

Maoni yako