Monday 23 March 2009

MOTO MOTO MOTO



Paradise Holiday Resort pamoja na Ocenic Bay zote zikiwa Bagamoyo zachomeka na moto mkubwa. Kwa mujibu wa shuhuda wetu moto huo ulianza eneo la Bistro Alakat Restaurant ambapo cheche za moto ziliwaka hadi kwenye makuti. Moto ukaenea kwenye Main Restaurant iliyo karibu na store ya chakula. Moto huo ulienea hoteli nzima na ikawa vigumu kuuzima. Magari ya zima moto yalichelewa kufika eneo la tukio kwa sababu yanatokea Dar es salaam. Hoteli hii ya kifahari imeteketea kabisa kilichobakia ni vibanda vitatu vya makuti katika eneo la bahari, Paradise Holiday Resort ilikuwa na vyumba tisini na tano. Moto huwo huo pia umeathiri Hoteli ya jirani ya Oceanic Bay, kiasi cha hasara hakijajulikana mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako