Friday 25 November 2016

TANZANIA YA VIWANDA

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alianzia ziara yake kwa kukagua uendeshaji wa Kiwanda wa cha tambi cha TanzaniaPasta, kilichopo eneo la Viwanda, Vingunguti wilayani Ilala. akizungungumza alipongeza hatua ya kuanzishwa kiwanda hicho akisema kinachangia lengo la Rais John Magufuli la kutaka Tanzania ijayo kuwa ya viwanda kwa lengo la kukuza nakuimarisha uchumi wa Taifa.
Hata hivyo aliutaka uongozi wa Kiwanda hicho kuhakikisha kinatimiza masharti ya utunzaji mazingira ikiwa ni pamoja na kutotiririsha maji hovyo, na pia kuhakikisha wananchi waliokusudiwa kulipwa ili kuondoka karibu na kiwanda wanafanyiwa hivyo mapema.
Pia aliwaasa wananchi kusisitiza watoto wao kusoma masomo ya sayansi kwa kuwa kazi nyingi za viwandani zinafanywa na masomi wa somo hilo, na kwamba vinginevyo atakaoajiriwa bila kuwa na elimu ya sayansi watabaki kuwa waokota maboksi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia malighafi zinazotumika kuzalishia mafuta ya kupikia kutoka kiwanda cha Mt. Meru Miller mjini Arusha
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda akigangua viwanda vya Paper Kraft kilichopo na cha Tanzania Tooku vilivyopo Mabibo Extenal leo jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Maoni yako