Wednesday 9 November 2016

HOT NEWS; WAMAREKANI WAPIGA KURA KUMCHAGUA RAIS MPYA

Donald Trump na Hillary Clinton wagombea katika uchaguzi wa urais Marekani, Novemba 8, 2016.
Wananchi wa Marekani watapiga kura leo Jumanne kumchagua rais wao, ambaye atamrithi Rais Barack Obama. Wagombea katika uchaguzi huo ni Donald Trump wa chama cha Republicana na Hillary Clinton wa chama cha Democratic.
Uchaguzi huu umekua na ushindani mkubwa tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi mpaka siku ya leo ya uchaguzi watu wameendelea kutoa tathmini zao kuhusu nani ataibuka mshindi.
Awali wagombea hawa wawili walionekana katika mijadala kwenye runinga wakitupia vijembe na kila mmoja kumshutumu mwengine kwa makosa aliyofanya kwamba hana hadhi ya kuliongoza taifa la Marekani.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako