Sunday 27 November 2016

KAMPUNI YA MURO KUUZA MABASI NA MALI ZAKE NYINGINE

Kwa siku za hivi karibuni kumekuwepo na ongezeko kubwa la nyumba kipigwa mnada, viwanja, magari, hoteli na mali mbalimbali kutokana na sababu mbalimbali kubwa ikiwa ni baadhi wa wakopaji kushindwa kurejesha fedha za mikopo walizochukua kutoka katika taasisi za kifedha.

Mbali na kupigwa mnada, baadhi ya hoteli na kumbi nyingine zimebadilishwa matumizi ambapo nyingi zimefanywa hosteli kwa ajili ya wanafunzi wa vyuo huku nyingine zikibadilishwa na kuwa shule na vyuo wakati wamiliki wengine wakiamua kuzifunga au kupunguza idadi ya wafanyakazi.

Kampuni ya Muro Investiment Co. Ltd inayomiliki mabasi ya safari za mikoani na vituo vya kuwekea mafuta imetangaza kuuza mali hizo. Kampuni hiyo haikueleza sababu za kuuza mali hizo.

Hili hapa chini ndilo tangazo la kampuni hiyo likielezea mali zinazouzwa.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako