Sunday 27 April 2014

MWEMBE WA MUUNGANO NAO WATIMIZA MIAKA 50

Wakati wa Sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tarehe 26 Aprili 1964, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Rais wa Zanzibar Abeid Amaan Karume ambao sasa wote ni marehemu, walipanda katika shimo moja miembe miwili mmoja kutoka Zanzibar na mwingine kutoka Tanganyika. Miembe hiyo imekuwa na kustawi pamoja na kufanya shina moja 'through grafting' .Leo hii mti huo wa mwembe umestawi vyema katika bustani ya Ikulu, Dar es Salaam, kama unavyoonekana leo Aprili 26, 2014 ambayo ni Siku ya miaka 50 ya Muungano.
(Picha na maelezo kwa hisani ya CCM Blog)

1 comment:

Maoni yako