Friday, 6 March 2015

UKATILI DHIDI YA NDUGU ZETU ALBINO:MAKALI YA SHERIA

Na hawa wanne hapa chini wamehukumiwa kifo kufuatia kumuua Zawadi Magimbu (32) mlemavu wa ngozi huko Geita.
Kutoka kushoto ni Nasoro Charles, Singu Siantemi, Masaru Kahindi na Ndahanya Lumola. Picha na Jackline Masinde.

HALI HII MPAKA LINI?

Abiria wakigombania kuingia kuingia kwenye daladala hadi wengine wanapitia mlango wa dereva. Hii ni hatari na sio jambo la busara. Tunaomba Serikali izidi kuongeza nguvu kutatua tatizo hili

JK AKUTANA NA VIONGOZI WA WENYE ULEMAVU WA NGOZI-ALBINO

Rais Kikwete akiongea na ​Viongozi wa Chama Cha Albino Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam Alhamisi Machi 5, 2015 alipowakaribisha ili kusikiliza matatizo yao na kujadiliana nao mikakati ya namna ya kukomesha ukatili na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini.
(Picha kwa hisani ya Le Mutuz Blog)

Thursday, 5 March 2015

MVUA YA MAAFA SHINYANGA

Mwananchi huko Kahama Shinyanga akiwa amebeba bonge la barafu lililofanyika kutokana na mvua ya mawe ya barafu ilonyesha mkoani hapo na kuleta maafa makubwa. Pole kwa wafiwa wote, tunawaombea majeruhi wapatenafuu na wote walioathirika na maafa hayo wapate nafuu ya maisha baada ya maafa hayo

JITAMBUA

Pamoja na hali ngumu ya maisha, lakini isifanye na ustaarabu nao kuuweka pembeni katika jambo lolote hata lile unaloliona ni dogo

Monday, 2 March 2015

CHELSEA MABINGWA "CAPITAL ONE"

Kocha wa Chelsea Jose Morinho akifurahia ushindi huo
Wachezaji wa Chelsea wakiwa wenye furaha kwa ushindi wa Capital One

WIKI YA UTAFUTAJI IMEANZA TENA

Baada ya mapumziko ya mwisho wa Juma ambapo pia ulikuwa ni mwisho wa Mwezi Februari, sasa tumeanza juma la kwanza la mwezi Machi. Nawatakia wote utafutaji mwema iwe shuleni, kazini au popote pale.
Mambo ya Kilimo kwanza yamefika mpaka Umasaini.
Uvuvi
Wafanyakazi wa Kiwandani wanapotenga muda wao ili kufanya usafi wa mazingira

Sunday, 1 March 2015

JUMAPILI YATANDA GIZA KUFUATIA KIFO CHA KEPTENI KOMBA

Mhe Rais Jakaya Kikwete na viongozi wengine wa Chama na Serikali na wananchi wengine wamekuwa wakimiminika nyumbani kwa Hayati Komba huko Mbezi Tangi Bovu Dar ili kutoa pole kwa wafiwa. Hakika wanaCCM na wanaTOT kwa namna ya pekee wamepoteza moja ya nguzo zao muhimu. Maombolezo bado yananendelea na kesho Mwili wa Hayati Komba utasafirishwa kwenda Ruvuma kwa mazishi.
Mhe.Rais Kikwete akitia sahihi kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Marehemu Komba
Mhe.Rais Kikwete akimfariji mke wa Marehemu ndg.Salome Komba