Tuesday 31 May 2016

WANAFUNZI WA CHUO KIKUU DAR-UDSM WAFANYA MGOMO

Wakati ambapo Wanafunzi wanaosomea kozi ya Ualimu wa Sayansi katika Chuo Kikuu cha Dodoma kuamriwa waondoke Chuoni hapo, leo baadhi ya wanafunzi wa UDSM wamefanya mgomo kudai fedhha za kujikimu.
Wanafunzi wa chuo kikuu cha cha Dar es salaam mpaka sasa wamegoma wakiishinikiza bodi ya mikopo kutoa fedha kwa ajili ya kujikimu.

Makamu wa Rais wa serikali ya wanafunzi, Shamila Mshengema amesema mgomo huo ni matokeo ya taarifa zisizoeleweka zilizo kuwa zikitolewa na bodi juu ya lini fedha hizo zitatolewa.

Kwa kawaida pesa ya chakula huingiziwa kila baada ya siku 60 na mpaka sasa yapata wiki mbili pesa hiyo haijaingizwa

Mgomo huo unakuja zikiwa zimebaki siku mbili kabla ya Rais Magufuli Kuzulu chuo hicho kwa ajili ya uzinduzi wa jengo la Maktaba.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako