Sunday 17 March 2013

TAFAKARI YA LEO

MAMBO 30 YANAYOKUONYESHA KUWA SASA UMRI UMEKUTUPA
MKONO....ushakuwa mtu mzima...:

1. Huna muda wa kushinda na
mpenzi wako kutwa nzima mkipiga
stori za mapenzi
2. Ukihitaji kufanya mapenzi mahali
unakokufikiria ni kitandani
3. Unaanza kujaza friji lako kwa
vyakula zaidi kuliko pombe
4. Muziki unaoupenda unausikia
ukiwa kwenye lifti ama kwenye gari
lako ukienda na kutoka kazini
5. Saa 11 alfajiri ndiyo muda
unaoamka, na siyo muda tena
unaorudi kulala
6. Unatazama taarifa ya habari hadi
utabiri wa hali ya hewa
7. Rafiki zako wanakualika zaidi
kwenye vikao vya harusi kuliko
mtoko wa kwenda Maisha Club
8. Ukienda dukani kununua kitu
unakuwa na juhudi sana ya kuomba
upunguziwe bei
9. Idadi ya tisheti na jinsi inapungua
kwa kasi kwenye kabati lako la nguo
10.Wewe ndiyo unayekumbuka
kuwapigia simu polisi endapo
mtaani kwenu kuna vijana wavuta
bangi wanaowasumbua
11. Ndugu zako watu wazima
wanajisikia kawaida tu kufanya utani
wa kiutu uzima mbele yako
12. Hukumbuki tena Azam Ice
Cream na Samaki Samaki wanafunga
saa ngapi
13. Timu yako ya mpira ikifungwa
hutaki tena kutaniwa na watu
14. Wanyama uwapendao kama
mbwa na paka unawaandalia chakula
kwa kanuni za kisayansi badala ya
kuwapa mabaki uliyotoka nayo
Subway ama Steers
15. Ukilala kwenye kochi unaamka
mgongo unakuuma sana
16. Unaithamini sana ratiba yako ya
kulala
17. Ukiwa nyumbani unaanza
kutumia muda wako wa ziada
kulima lima bustani ya maua ama
mbogamboga badala ya kutazama
filamu na kuzurura
18. Kila kitu kikinunuliwa nyumbani
jambo la kwanza unalouliza,
"Umenunua sh' ngapi?"
19. Unakwenda duka la madawa
kununua Ibuprofen na Antacid, siyo
kondomu tena wala kipima mimba
20. Unaanza kununua magazeti ya
Mwananchi, The Express, Citizen na
Nipashe badala ya Uwazi, Ijumaa,
Kiu na Amani
21. Unapata kifungua kinywa kwa
wakati
22. Ukiwa baa unanunua bia
unazohitaji wewe badala ya kusema
"zungusha kama tulivyo"
23. Asilimia 90 ya muda unaoutumia
kwenye kompyuta yako unautumia
kufanya kazi badala ya kuchati
24. Ukijisikia hamu ya kunywa kilevi
unaanza kunywea nyumbani ili
kupunguza gharama kabla hujaenda
baa
25. Ukimwona rafiki yako yu
mjamzito unampongeza sana badala
ya kumwuliza, "imekuwaje tena?"
26. Ukienda kutembea mahali
unaulizia bei za viwanja
27. Hupendi tena kuwaazimisha
marafiki zako magari yako
28. Ukiwa na rafiki zako unapenda
kujadiliana nao kuhusiana na
mfumuko wa bei na mfumo mbovu
wa utawala
29. Ukiwa unakula chakula unakuwa
mkali ikitokea chakula kimewekwa
mafuta mengi ama chumvi nyingi
30. Ukimaliza kusoma kanuni hizo
29 hapo juu unaanza kuhesabu
ambazo unaingia wewe.
Ukiona una nusu ya sifa hizi 30 basi
huhitaji kupigiwa kengele
kukumbushwa kuwa umri
ushayoyooooooooooooooooooo

1 comment:

Maoni yako