Tuesday 5 March 2013

MOTO-LEO

Moto umetokea tena leo na kuunguza baadhi ya ghala katika eneo la Uwekezaji la Shekilango Jijini DAR. Bado haijajulikana vizuri moto huo ulianzia wapi, ila mpaka picha hii inapigwa bado moto huo ulikuwa haujaweza kuzimwa kutokana na moshi mweusi kutanda juu ya eneo hilo na kusababisha usumbufu wa wahusika wa zima moto. Ikumbukwe kuwa moto huu unatokea baada ya tukio kama hili kutokea huko Mbezi- Kiwanda cha Chemi and Cotex, Mwenge madukani kwenye kituo cha Daladala na juzi tu huko Tegeta.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako