Saturday, 31 December 2016
TAHADHARI: KWA JOTO HILI .......
Jamani naomba nitoe tahadhari.
Jua limekuwa kali mno na joto kuongezeka sana hasa Dar na kwingineko..viumbe hai vinahangaika makazi hayakaliki...nyoka, nge, tandu ambao si rahisi kuwasikia wanatembea au kutambaa au hata kuwaona wakiwa mbali, wanatafuta maeneo tofauti ya kujihifadhi na hasa kupenya kwenye makazi..nyumba zetu. Mnatahadharishwa kuhakikisha milango na madirisha vimefungwa vema wakati wote kuzuia wasipenye..nyumba zipigwe dawa ndani na nje. jua ni kali na maeneo mengi yana ukame kipindi hiki.
Hii picha ya mamba ni ya leo leo pande za Kigamboni Mwongozo ,amekutwa akizagaa kitaa wananch wakamshughulkia
Jua limekuwa kali mno na joto kuongezeka sana hasa Dar na kwingineko..viumbe hai vinahangaika makazi hayakaliki...nyoka, nge, tandu ambao si rahisi kuwasikia wanatembea au kutambaa au hata kuwaona wakiwa mbali, wanatafuta maeneo tofauti ya kujihifadhi na hasa kupenya kwenye makazi..nyumba zetu. Mnatahadharishwa kuhakikisha milango na madirisha vimefungwa vema wakati wote kuzuia wasipenye..nyumba zipigwe dawa ndani na nje. jua ni kali na maeneo mengi yana ukame kipindi hiki.
Hii picha ya mamba ni ya leo leo pande za Kigamboni Mwongozo ,amekutwa akizagaa kitaa wananch wakamshughulkia
Friday, 30 December 2016
2017 BEI YA UMEME KUPANDA
Bei za umeme zimepanda kwa 8.5% badala ya 18.19% iliyopendekezwa na TANESCO.
Ongezeko la bei ya huduma za umeme limetokana na kuzidi kwa gharama za uzalishaji wake.
Shirika la umeme Zanzibar (ZECO) ambalo linanunua umeme wa jumla kupeleka Zanzibar limeongezewa 5.7% ya bei ya umeme.
Ongezeko hilo halitaathiri wateja wa majumbani ambao matumizi yao hayazidi uniti 75 kwa mwezi.
Kundi la TIb linalohusisha viwanda vidogo,mabango na minara ya mawasiliano litakua na tozo ya mwezi ya shilingi 5,520.
Bei hizo zitaanza kutumika Januari Mosi mwaka 2017.
TANESCO inatarajia kufanya maboresho ya msongo wa umeme na kutekeleza miradi mipya ya kuunganisha wateja ili kuboresha huduma za umeme.
IMEANDALIWA NA IDARA YA HABARI (MAELEZO)
Ongezeko la bei ya huduma za umeme limetokana na kuzidi kwa gharama za uzalishaji wake.
Shirika la umeme Zanzibar (ZECO) ambalo linanunua umeme wa jumla kupeleka Zanzibar limeongezewa 5.7% ya bei ya umeme.
Ongezeko hilo halitaathiri wateja wa majumbani ambao matumizi yao hayazidi uniti 75 kwa mwezi.
Kundi la TIb linalohusisha viwanda vidogo,mabango na minara ya mawasiliano litakua na tozo ya mwezi ya shilingi 5,520.
Bei hizo zitaanza kutumika Januari Mosi mwaka 2017.
TANESCO inatarajia kufanya maboresho ya msongo wa umeme na kutekeleza miradi mipya ya kuunganisha wateja ili kuboresha huduma za umeme.
IMEANDALIWA NA IDARA YA HABARI (MAELEZO)
Thursday, 29 December 2016
Wednesday, 28 December 2016
MAAMUZI YA RUFAA YA KESI YA MHE GODBLESS LEMA KUJULIKANA JAN 4,2017
Na.Vero Ignatus Arusha.
Mahakama kuu kanda ya Arusha imesikiliza maombi ya rufaa yayaliyowasilishwa na upande wa jamhuri na ule wa mshtakiwa Godbless Lema ambapo pande zote mbili wamekubaliana kusikilizwa rufaa ya upande wa jamhuri ambapo upande wa serikali wameiomba mahakama kuwasilisha kwa hati ya maandishi hapo kesho tarehe 30 disemba 2016
Aidha rufaa hizo ni pamoja na ile ya upande wa Jamhuri kutoridhika na maamuzi ya Jaji Dkt. Modesta Opiyo la kuwapa siku kumi (10) upande wa mshtakiwa Lema kufaili notisi ya rufaa ,na upande wa mshtakiwa ni ile ya kupinga uamuzi wa mahakama ya chini kushindwa kumpa Lema masharti ya dhamana
Jaji aliyekuwa anasikiliza kesi ya rufaa hizo Salma Magimbi amesema kuwa mara baada ya upande wa jamhuri kuleta rufaa kwa njia ya maandishi upande wa mshtakiwa Lema wataijibu tarehe 30 desemba 2016 ambapo tarehe 2 januari watakutana pande zote kwa ajili ya kufanya majumuisho na maamuzi ya rufaa hiyo yatatolewa tarehe 4 januari 2017
Hata hivyo baada ya kusikiliza rufaa hizo mahakama imeibua hoja yenyewe na kuwapa kazi mawakili wa pande zote mbili kuangalia kuwa notisi iliyowasilishwa na mahakama ya chini imekidhi matakwa ya kisheria?
Kwa upande wa wakili wa mshtakiwa Peter Kibatala amesema kuwa kwa upande wao wameiomba mahakama kusubirisha rufaa yao ili wasikilize kwanza rufaa ya upande wa jamhuri kwani rufaa zote zimegongana na zinaelekea sehemu moja
"Unajua leo rufaa mbili zimegongana ile ya upande wa jamhuri na ile ya kwetu sisi,hivyo basi sisis tumeiomba mahakama kusitisha rufaa yetui isikilizwe ile ya serikali kwanza,kwani rufaa zote zinaelekea upandemmoja ,wandege apande ndege na wa basi apande basi "alisema Kibatala.
Hata hivyo mbunge huyo wa Arusha mjini Godbless Lema amerudishwa rumande hadi hapo maamuzi yatakapotolewa na mahakama.
Mahakama kuu kanda ya Arusha imesikiliza maombi ya rufaa yayaliyowasilishwa na upande wa jamhuri na ule wa mshtakiwa Godbless Lema ambapo pande zote mbili wamekubaliana kusikilizwa rufaa ya upande wa jamhuri ambapo upande wa serikali wameiomba mahakama kuwasilisha kwa hati ya maandishi hapo kesho tarehe 30 disemba 2016
Aidha rufaa hizo ni pamoja na ile ya upande wa Jamhuri kutoridhika na maamuzi ya Jaji Dkt. Modesta Opiyo la kuwapa siku kumi (10) upande wa mshtakiwa Lema kufaili notisi ya rufaa ,na upande wa mshtakiwa ni ile ya kupinga uamuzi wa mahakama ya chini kushindwa kumpa Lema masharti ya dhamana
Jaji aliyekuwa anasikiliza kesi ya rufaa hizo Salma Magimbi amesema kuwa mara baada ya upande wa jamhuri kuleta rufaa kwa njia ya maandishi upande wa mshtakiwa Lema wataijibu tarehe 30 desemba 2016 ambapo tarehe 2 januari watakutana pande zote kwa ajili ya kufanya majumuisho na maamuzi ya rufaa hiyo yatatolewa tarehe 4 januari 2017
Hata hivyo baada ya kusikiliza rufaa hizo mahakama imeibua hoja yenyewe na kuwapa kazi mawakili wa pande zote mbili kuangalia kuwa notisi iliyowasilishwa na mahakama ya chini imekidhi matakwa ya kisheria?
Kwa upande wa wakili wa mshtakiwa Peter Kibatala amesema kuwa kwa upande wao wameiomba mahakama kusubirisha rufaa yao ili wasikilize kwanza rufaa ya upande wa jamhuri kwani rufaa zote zimegongana na zinaelekea sehemu moja
"Unajua leo rufaa mbili zimegongana ile ya upande wa jamhuri na ile ya kwetu sisi,hivyo basi sisis tumeiomba mahakama kusitisha rufaa yetui isikilizwe ile ya serikali kwanza,kwani rufaa zote zinaelekea upandemmoja ,wandege apande ndege na wa basi apande basi "alisema Kibatala.
Hata hivyo mbunge huyo wa Arusha mjini Godbless Lema amerudishwa rumande hadi hapo maamuzi yatakapotolewa na mahakama.
Tuesday, 27 December 2016
UJENZI WA JULIUS NYERERE I AIRPORT WAFIKIA ASILIMIA 65
Tume ya mipango imefanya ziara katika mradi wa ujenzi wa jengo la III la abiria katika uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (Terminal III) jijini Dar es Salaam kwa lengo la kukagua maendeleo ya mradi huo na kuelezwa kuwa ujenzi umefikia asilimia 65.
Akitoa maelezo mbele ya timu ya wataalamu kutoka Tume ya Mipango, Meneja wa Mradi huo Mhandisi Mwanaidi Mkwizu alieleza kuwa ujenzi huo unaotekelezwa na Mkandarasi wa kampuni ya BAM kutoka Uholanzi ulioanza Juni 2013 na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba Mwaka 2017.
Akielezea miundombinu ya uwanja huo, Mhandisi Mkwizu alisema kuwa uwanja huo wa kisasa una barabara ya kuruka ndege (runway) yenye urefu wa kilometa 3 na upana wa mita 60 ambapo upana unaohitajika kwa matumizi ya ndege ni mita 45.
Aliongeza kuwa mradi huo pia umeangalia changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara na kuamua kutafua vyanzo mbalimbali ili kuondokana na utegemezi wa chanzo kimoja ambacho kinaweza kukwamisha shughuli katika uwanja huo pale inapotokea hitilafu.
Alieleza kuwa kutakuwa na njia mbili tofauti za kuleta umeme kutoka TANESCO ambapo njia moja ni kwa ajili ya dharura na pia endapo kutakuwa na tatizo la kukatika umeme kupitia njia za TANESCO, umeme utapatikana kutoka chanzo mbadala cha dharura kwa kutumia jenerata nne kubwa za kisasa za dizeli zilizopo eneo la mradi ambazo zinatosha kukidhi mahitaji ya eneo hilo.
Alisisitiza kuwa tayari wamefanya mazungumzo na TANESCO na kukubaliana kuwa njia hizo za umeme ni kwa ajili ya uwanja huo pekee na hakuna wateja wengine watakaounganishiwa katika njia hizo.
Mhandisi mkwizu alimalizia kwa kusema kuwa yeye pamoja na timu yake ya wataalamu wanaendelea kufanya usimamizi wa karibu ili kuhakikisha kuwa utekelezaji wa mradi huo unaenda sambamba na malengo yaliyopangwa.
Wataalamu wa ukaguzi wa miradi kutoka Tume ya Mipango walipata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya ujenzi wa mradi huo na kuonesha kuridhishwa na kasi yautekelezaji huku wakimshauri menejea wa mradi huo kuendelea na ufanisi wake katika kusimamia kazi hiyo ili kuhakikisha malengo ya mradi huo yanafikiwa.
Akitoa maelezo mbele ya timu ya wataalamu kutoka Tume ya Mipango, Meneja wa Mradi huo Mhandisi Mwanaidi Mkwizu alieleza kuwa ujenzi huo unaotekelezwa na Mkandarasi wa kampuni ya BAM kutoka Uholanzi ulioanza Juni 2013 na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba Mwaka 2017.
Akielezea miundombinu ya uwanja huo, Mhandisi Mkwizu alisema kuwa uwanja huo wa kisasa una barabara ya kuruka ndege (runway) yenye urefu wa kilometa 3 na upana wa mita 60 ambapo upana unaohitajika kwa matumizi ya ndege ni mita 45.
Aliongeza kuwa mradi huo pia umeangalia changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara na kuamua kutafua vyanzo mbalimbali ili kuondokana na utegemezi wa chanzo kimoja ambacho kinaweza kukwamisha shughuli katika uwanja huo pale inapotokea hitilafu.
Alieleza kuwa kutakuwa na njia mbili tofauti za kuleta umeme kutoka TANESCO ambapo njia moja ni kwa ajili ya dharura na pia endapo kutakuwa na tatizo la kukatika umeme kupitia njia za TANESCO, umeme utapatikana kutoka chanzo mbadala cha dharura kwa kutumia jenerata nne kubwa za kisasa za dizeli zilizopo eneo la mradi ambazo zinatosha kukidhi mahitaji ya eneo hilo.
Alisisitiza kuwa tayari wamefanya mazungumzo na TANESCO na kukubaliana kuwa njia hizo za umeme ni kwa ajili ya uwanja huo pekee na hakuna wateja wengine watakaounganishiwa katika njia hizo.
Mhandisi mkwizu alimalizia kwa kusema kuwa yeye pamoja na timu yake ya wataalamu wanaendelea kufanya usimamizi wa karibu ili kuhakikisha kuwa utekelezaji wa mradi huo unaenda sambamba na malengo yaliyopangwa.
Wataalamu wa ukaguzi wa miradi kutoka Tume ya Mipango walipata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya ujenzi wa mradi huo na kuonesha kuridhishwa na kasi yautekelezaji huku wakimshauri menejea wa mradi huo kuendelea na ufanisi wake katika kusimamia kazi hiyo ili kuhakikisha malengo ya mradi huo yanafikiwa.
UDAKU; HUYU NDIE MKE MTARAJIWA WA AY
Mwanamuziki Ay kwa mara ya kwanza amemtambulisha rasmi Mpenzi wake....
Habari hii Leo imekuwa gumzo mitandaoni kwa wengi walikuwa wakijiuliza Ay mpenzi wake ni nani hasa baada ya Swahiba wake wa Karibu Mwana FA Kuoa....
Habari hii Leo imekuwa gumzo mitandaoni kwa wengi walikuwa wakijiuliza Ay mpenzi wake ni nani hasa baada ya Swahiba wake wa Karibu Mwana FA Kuoa....
Monday, 26 December 2016
Subscribe to:
Posts (Atom)