NAULI ZA DART ZIMEJALI ZAIDI VIPATO VYA WALALA HOI
Zimetangazwa Rasmi 09/05/2016
1. Wanafunzi 200/=
2. Feeder 400/=
3. Trunk 650/=
4. Trunk/Feeder 800/=
TAFSIRI.
1. WANAFUNZI INAELEWEKA.
2. TRUNK Sh. 650/= Ni pale utakapokuwa umepanda Basi la DART linalopita kwenye Njia maalumu.Mfano Kuanzia Kimara - Kivukoni, Kimara- Kariakoo, Moroco - Kivukoni, Morocco - Kariakoo. Hii haijalishi unapita vituo vingapi au unashukia kituo gani kama ilivyo kwenye Daladala.
3. Feeder Sh. 400/= Ni pale utakapo panda Basi la DART ambalo linafanya kazi nje ya Mfumo (Barabara Maalum za DART). Mfano Kimara - Mbezi.
4. Trunk/Feeder sh. 800/= hapa ni pale utakapo tumia Aina zote za Usafiri Kwa kuunganisha Mfano Mbezi Kimara Halafu Kimara Posta.
DART USAFIRI WA HARAKA NA UHAKIKA
Tuesday, 10 May 2016
Sunday, 8 May 2016
Wednesday, 4 May 2016
DKT ASHA ROSE MIGIRO BALOZI MPYA WA TANZANIA UINGEREZA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Asha-Rose Migiro kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza.
Dkt. Asha-Rose Migiro anakwenda kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Peter Kalaghe ambaye amerudishwa nyumbani.
Dkt. Asha-Rose Migiro ataapishwa kesho Alhamisi tarehe 05 Mei, 2016 katika Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma
04 Mei, 2016
-------------------------------
Mapito ya Dk. Migiro
Dk. Migiro alizaliwa tarehe 9 Julai 1956 katika Wilaya ya Songea, Ruvuma. Alisoma Shule ya Msingi Mnazi Mmoja, Dar es Salaam mwaka 1963 hadi mwaka 1966.
Dk. Migiro alihamia Shule ya Msingi Korogwe, Tanga ambapo aliendela na elimu ya msingi mwaka 1967–1969.
Baadaye akajiunga kidato cha kwanza mpaka cha nne katika Shule ya Sekondari Weruweru, Kilimanjaro mwaka 1970 hadi 1973 na Kidato cha Tano na Sita katika Shule ya Sekondari Korogwe mwaka 1974 -1975.
Dk. Migiro alikuwa mmoja wa wasichana waliofaulu vizuri Korogwe Sekondari na alipojiunga Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka 1977, alichukua masomo ya sheria na kuhitimu Shahada yake (LLB) mwaka 1980.
Baadaye aliajiriwa UDSM kufundisha masomo ya sheria kama Mhadhiri Msaidizi. Alifanya kazi hiyo kwa miaka miwili kabla ya kuendelea tena na masomo ya juu ya sheria mwaka 1982–1984 hapohapo UDSM na kutunukiwa shahada ya uzamili (LLM).
Kati ya mwaka 1985–1988, alifundisha UDSM. Mwaka 1988 alikwenda Chuo Kikuu cha Konstanz, Ujerumani ambako alisoma na kutunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika masuala ya Sheria mwaka 1992.
Dk. Migiro alirejea Tanzania akiwa Mhadhiri Mwandamizi na aliendelea kufundisha katika Kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hadi mwaka 2000 alipoingia kwenye siasa.
Akiwa UDSM kati ya mwaka 1992 – 1994 Dk. Migiro alikuwa Mkuu wa Idara ya Sheria za Katiba na Utawala.
Kati ya mwaka 1994 – 1997 aliongoza Idara ya Sheria za Makosa ya Jinai (Idara zote zipo katika Kitivo cha Sheria UDSM).
Dk Migiro ni mzungumzaji mzuri katika lugha ya Kiingereza, Kifaransa na Kijerumani. Ni mke wa Profesa Cleophas Migiro na wana watoto wawili wa kike.
Dk Migiro alianza na siasa za kujijenga akitokea katika taaluma. Mwaka 2000, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa alimteua kuwa waziri kwenye Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto.
Alitumikia wadhifa huo hadi mwaka 2005 bila kubadilishwa akisimamia mambo mengi ya kisera na kimiundombinu, bila kusahau utekelezaji na upiganiaji wa haki za wanawake na watoto.
Rais Jakaya Kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005, alimteua kuwa Mbunge na Waziri wa Mambo ya Nje, Januari 2006 na kuwa mwanamke wa kwanza kuwahi kushikilia wadhifa huo. Katika kipindi cha mwaka mmoja tu, alifanya kazi nyingi za kimataifa zilizomweka katika anga nyingine kisiasa.
Januari 5, 2007, aliteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu (UN) mpaka 2012 alipomaliza muda wake. Januari mwaka 2013, Dk Migiro aliteuliwa kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) na Desemba 2013 aliteuliwa kuwa mbunge katika Bunge la Tanzania.
Januari 2014 aliteuliwa kuwa Waziri wa Sheria na Katiba, nafasi ambayo alidumu nayo mpaka Rais Kikwete alipomaliza muda wake mwaka jana.
Dkt. Asha-Rose Migiro anakwenda kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Peter Kalaghe ambaye amerudishwa nyumbani.
Dkt. Asha-Rose Migiro ataapishwa kesho Alhamisi tarehe 05 Mei, 2016 katika Ikulu ndogo ya Chamwino Mkoani Dodoma.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma
04 Mei, 2016
-------------------------------
Mapito ya Dk. Migiro
Dk. Migiro alizaliwa tarehe 9 Julai 1956 katika Wilaya ya Songea, Ruvuma. Alisoma Shule ya Msingi Mnazi Mmoja, Dar es Salaam mwaka 1963 hadi mwaka 1966.
Dk. Migiro alihamia Shule ya Msingi Korogwe, Tanga ambapo aliendela na elimu ya msingi mwaka 1967–1969.
Baadaye akajiunga kidato cha kwanza mpaka cha nne katika Shule ya Sekondari Weruweru, Kilimanjaro mwaka 1970 hadi 1973 na Kidato cha Tano na Sita katika Shule ya Sekondari Korogwe mwaka 1974 -1975.
Dk. Migiro alikuwa mmoja wa wasichana waliofaulu vizuri Korogwe Sekondari na alipojiunga Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka 1977, alichukua masomo ya sheria na kuhitimu Shahada yake (LLB) mwaka 1980.
Baadaye aliajiriwa UDSM kufundisha masomo ya sheria kama Mhadhiri Msaidizi. Alifanya kazi hiyo kwa miaka miwili kabla ya kuendelea tena na masomo ya juu ya sheria mwaka 1982–1984 hapohapo UDSM na kutunukiwa shahada ya uzamili (LLM).
Kati ya mwaka 1985–1988, alifundisha UDSM. Mwaka 1988 alikwenda Chuo Kikuu cha Konstanz, Ujerumani ambako alisoma na kutunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika masuala ya Sheria mwaka 1992.
Dk. Migiro alirejea Tanzania akiwa Mhadhiri Mwandamizi na aliendelea kufundisha katika Kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hadi mwaka 2000 alipoingia kwenye siasa.
Akiwa UDSM kati ya mwaka 1992 – 1994 Dk. Migiro alikuwa Mkuu wa Idara ya Sheria za Katiba na Utawala.
Kati ya mwaka 1994 – 1997 aliongoza Idara ya Sheria za Makosa ya Jinai (Idara zote zipo katika Kitivo cha Sheria UDSM).
Dk Migiro ni mzungumzaji mzuri katika lugha ya Kiingereza, Kifaransa na Kijerumani. Ni mke wa Profesa Cleophas Migiro na wana watoto wawili wa kike.
Dk Migiro alianza na siasa za kujijenga akitokea katika taaluma. Mwaka 2000, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa alimteua kuwa waziri kwenye Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto.
Alitumikia wadhifa huo hadi mwaka 2005 bila kubadilishwa akisimamia mambo mengi ya kisera na kimiundombinu, bila kusahau utekelezaji na upiganiaji wa haki za wanawake na watoto.
Rais Jakaya Kikwete alipoingia madarakani mwaka 2005, alimteua kuwa Mbunge na Waziri wa Mambo ya Nje, Januari 2006 na kuwa mwanamke wa kwanza kuwahi kushikilia wadhifa huo. Katika kipindi cha mwaka mmoja tu, alifanya kazi nyingi za kimataifa zilizomweka katika anga nyingine kisiasa.
Januari 5, 2007, aliteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu (UN) mpaka 2012 alipomaliza muda wake. Januari mwaka 2013, Dk Migiro aliteuliwa kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) na Desemba 2013 aliteuliwa kuwa mbunge katika Bunge la Tanzania.
Januari 2014 aliteuliwa kuwa Waziri wa Sheria na Katiba, nafasi ambayo alidumu nayo mpaka Rais Kikwete alipomaliza muda wake mwaka jana.
KIKWETE: "WANAFUNZI CHAGUENI KOZI ZENYE AJIRA KIRAHISI"
RAIS Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, amewasaa wanafunzi kuchagua kozi zitakazowapatia ajira wanapo hitimu masomo yao.
Akizungumza katika mahafali ya 10 ya kidato cha sita katika Shule ya Sekondari Baobab, wilayani Bagamoyo, mkoa wa Pwani juzi, Kikwete alisema wimbi kubwa la vijana wasio na ajira limechangiwa na uchaguzi mbaya wa kozi ambazo haziendani na soko la ajira la sasa.
“Nawasaa kuwa makini katika kuchagua kozi zinazoendana na soko la jira ndani na nje ya nchi ili muweze kuajiriwa na kujiajiri pindi mnapohitimu,” alisema.
Alisema zipo fursa mbalimbali ikiwamo za kibiashara katika soko la Afrika Mashariki, Afrika na Dunia, ambazo kama wahitimu watasoma kozi zinazoendana na fursa zilizopo watajikomboa na changamoto ya ukosefu wa ajira.
“Nimetembea nchi nyingi duniani na kuona fursa mbalimbali, ni vyema basi vijana wakawa wanafanya maamuzi sahihi ili waweze kutumia fursa hizo.”
“Vijana wengi wamekuwa wakichagua michepuo ya kozi ambazo haziendani na mahitaji ya soko la ajira na kuwafanya kushindwa kupata nafasi katika soko la ajira,” aliongeza kusema.
Aidha, Kikwete alizitaka shule na vyuo nchini kufundisha lugha kubwa duniani kama Kichina na Kifaransa ili kuwaongezea uwezo wahitimu kufanya kazi katika maeneo mbalimbali dunia.
Aidha, alizishauri shule kutoa mafunzo ya ujasiriliamali ili kupanua fikra za vijana na waweze kujitengenezea ajira wanapohitimu.
Naye Mkurugenzi wa Shule ya Baobab alisema shule hiyo imefanikiwa kutoa wahitimu 774 kwa kipindi cha miaka 10, ambao asilimia 95 walipata ufaulu wa kujiunga na vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Alitaja idadi ya wahitimu wa mwaka huu kuwa ni 244, wasichana 176 na wavulana 68.
Akizungumza katika mahafali ya 10 ya kidato cha sita katika Shule ya Sekondari Baobab, wilayani Bagamoyo, mkoa wa Pwani juzi, Kikwete alisema wimbi kubwa la vijana wasio na ajira limechangiwa na uchaguzi mbaya wa kozi ambazo haziendani na soko la ajira la sasa.
“Nawasaa kuwa makini katika kuchagua kozi zinazoendana na soko la jira ndani na nje ya nchi ili muweze kuajiriwa na kujiajiri pindi mnapohitimu,” alisema.
Alisema zipo fursa mbalimbali ikiwamo za kibiashara katika soko la Afrika Mashariki, Afrika na Dunia, ambazo kama wahitimu watasoma kozi zinazoendana na fursa zilizopo watajikomboa na changamoto ya ukosefu wa ajira.
“Nimetembea nchi nyingi duniani na kuona fursa mbalimbali, ni vyema basi vijana wakawa wanafanya maamuzi sahihi ili waweze kutumia fursa hizo.”
“Vijana wengi wamekuwa wakichagua michepuo ya kozi ambazo haziendani na mahitaji ya soko la ajira na kuwafanya kushindwa kupata nafasi katika soko la ajira,” aliongeza kusema.
Aidha, Kikwete alizitaka shule na vyuo nchini kufundisha lugha kubwa duniani kama Kichina na Kifaransa ili kuwaongezea uwezo wahitimu kufanya kazi katika maeneo mbalimbali dunia.
Aidha, alizishauri shule kutoa mafunzo ya ujasiriliamali ili kupanua fikra za vijana na waweze kujitengenezea ajira wanapohitimu.
Naye Mkurugenzi wa Shule ya Baobab alisema shule hiyo imefanikiwa kutoa wahitimu 774 kwa kipindi cha miaka 10, ambao asilimia 95 walipata ufaulu wa kujiunga na vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Alitaja idadi ya wahitimu wa mwaka huu kuwa ni 244, wasichana 176 na wavulana 68.
MWANAFUNZI GENTRUDE CLEMENT KUSOMESHWA NA TAASISI KIDATO CHA TANO NA SITA
Kwa kutambua umuhimu wa elimu kwa kizazi cha miaka ijayo, Taasisi ya Misaada ya Kijamii ya Hamisi Kigwangalla iliyoanzishwa na Naibu Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla imejitolea kumlipia ada Getrude Clement kwa masomo yake ya kidato cha tano na sita.
Uamuzi huo wa kumsomesha Getrude umekuja baada ya jana kukaribishwa kuongea kwenye kikao cha wabunge watetezi wa haki za watoto ambapo Getrude alipata nafasi ya kutoa historia yake ambayo iliwatoa baadhi ya wabunge machozi.
Getrude aliwaeleza wabunge historia yake na hali yake ya kimaisha na kusema kuwa baba yake ni kinyozi na mama yake anafanya biashara ndogo ndogo za nyanya na vitunguu lakini bado amekuwa akijtuma katika masomo yake ambapo kwa sasa yupo kidato cha tatu katika shule ya Sekondari Mnarani, Mwanza.
Baada ya kusema hivyo, ndipo Dkt. Kigwangalla aliamua kujitolea kumsaidia mtoto huyo ili aweze kujiendeleza zaidi kielimu na kufikia malengo yake na zaidi akiahidi kumsomesha katika shule za kisasa ili apate elimu bora zaidi.
“Kwa kuthamini kipaji chake na mchango wake na kutambua nafasi yangu kama Naibu Waziri kwenye Wizara inayosimamia mambo ya Watoto na kama mbunge na mzazi wa mabinti, lakini zaidi kama mtu kutoka kwenye background ya maisha ya chini na ninayethamini mchango wa elimu kwenye maisha yangu, nimeamua kujitolea kumsomesha kidato cha tano na cha sita kwenye shule za kisasa,
“Taasisi yangu ya misaada ya kijamii ya Hamisi Kigwangalla Development Foundation itamlipia ada za masomo yake ya high school,” alisema Dkt. Kigwangalla.
Getrude Clement ambaye ana miaka 16 amepata nafasi hiyo ya kipekee baada ya kupata nafasi ya kutoa hotuba kwa niaba ya watoto na vijana wengine duniani katika mkutano wa Umoja wa Mataifa ambapo alikaribishwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon na kusifiwa na watu mbalimbali duniani kutokana na hotuba yake nzuri.
Uamuzi huo wa kumsomesha Getrude umekuja baada ya jana kukaribishwa kuongea kwenye kikao cha wabunge watetezi wa haki za watoto ambapo Getrude alipata nafasi ya kutoa historia yake ambayo iliwatoa baadhi ya wabunge machozi.
Getrude aliwaeleza wabunge historia yake na hali yake ya kimaisha na kusema kuwa baba yake ni kinyozi na mama yake anafanya biashara ndogo ndogo za nyanya na vitunguu lakini bado amekuwa akijtuma katika masomo yake ambapo kwa sasa yupo kidato cha tatu katika shule ya Sekondari Mnarani, Mwanza.
Baada ya kusema hivyo, ndipo Dkt. Kigwangalla aliamua kujitolea kumsaidia mtoto huyo ili aweze kujiendeleza zaidi kielimu na kufikia malengo yake na zaidi akiahidi kumsomesha katika shule za kisasa ili apate elimu bora zaidi.
“Kwa kuthamini kipaji chake na mchango wake na kutambua nafasi yangu kama Naibu Waziri kwenye Wizara inayosimamia mambo ya Watoto na kama mbunge na mzazi wa mabinti, lakini zaidi kama mtu kutoka kwenye background ya maisha ya chini na ninayethamini mchango wa elimu kwenye maisha yangu, nimeamua kujitolea kumsomesha kidato cha tano na cha sita kwenye shule za kisasa,
“Taasisi yangu ya misaada ya kijamii ya Hamisi Kigwangalla Development Foundation itamlipia ada za masomo yake ya high school,” alisema Dkt. Kigwangalla.
Getrude Clement ambaye ana miaka 16 amepata nafasi hiyo ya kipekee baada ya kupata nafasi ya kutoa hotuba kwa niaba ya watoto na vijana wengine duniani katika mkutano wa Umoja wa Mataifa ambapo alikaribishwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon na kusifiwa na watu mbalimbali duniani kutokana na hotuba yake nzuri.
MTOTO MWANAHABARI GETRUDE CLEMENT AKARIBISHWA BUNGENI DODOMA
Getrude Clement mwenye umri wa miaka 16 ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu anayesoma shule ya Sekondari Mnarani iliyopo jijini Mwanza, leo amepata nafasi ya kufika bungeni Dodoma baada ya kupewa mwaliko wa Serikali
Hivi karibuni Getrude alihutubia viongozi mbalimbali wa dunia kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa uliohusu mabadiliko ya tabia nchi uliofanyika New York Marekani ambapo leo Bungeni amewahimiza Watanzania kutunza mazingira na kufuata maelekezo yanayotolewa na Serikali na wataalamu wa mazingira ili kuyatunza mazingira wanamoishi.
Mwanafunzi huyo amekaribishwa na kutambulishwa kwa wabunge leo mjini Dodoma kwa heshima ya kuliwakilisha vema taifa wakati wa utiaji saini makubaliano ya namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki moon alimkaribisha Getrude kwa viongozi hao na kusema “Ni furaha yangu kumualika Getrude Clement ambaye pia ni mwakilishi wa vijana anayeishi Tanzania na anaziwakilisha sauti za vijana”.
Hivi karibuni Getrude alihutubia viongozi mbalimbali wa dunia kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa uliohusu mabadiliko ya tabia nchi uliofanyika New York Marekani ambapo leo Bungeni amewahimiza Watanzania kutunza mazingira na kufuata maelekezo yanayotolewa na Serikali na wataalamu wa mazingira ili kuyatunza mazingira wanamoishi.
Mwanafunzi huyo amekaribishwa na kutambulishwa kwa wabunge leo mjini Dodoma kwa heshima ya kuliwakilisha vema taifa wakati wa utiaji saini makubaliano ya namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki moon alimkaribisha Getrude kwa viongozi hao na kusema “Ni furaha yangu kumualika Getrude Clement ambaye pia ni mwakilishi wa vijana anayeishi Tanzania na anaziwakilisha sauti za vijana”.
WIMBO WA CHURA WA SNURA WAFUNGIWA
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini toka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Zawadi Msalla (katikati) akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari (hawapopichani) wakati akitoa tamko la Serikali kuhusu kusitishwa kwa wimbo wa Msanii Snura Mushi ujulikanao kwa jina la Chura kwa kukiuka maadili kushoto ni Mwanasheria wa wizara hiyo Bw. Patrick Kipangula na kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utamaduni Bibi. Lily Beleko.
Monday, 2 May 2016
RAIS MAGUFULI AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Rais wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein kabla ya kuanza kikao cha Baraza la Mawaziri katika ukumbi wa TAMISEMI mjini Dodoma leo Mei 2, 2016.
Sunday, 1 May 2016
Subscribe to:
Posts (Atom)