Friday, 31 October 2014

KATUNI YA LEO

Tazama namna ushirikina unavyoleta ukatili dhidi ya ubinadamu.

Thursday, 30 October 2014

TUCHAPE KAZI ILA KWA UMAKINI

Chombo hiki kinachosaidia kuingiza kipato hakika hakitumiki vizuri. Kama kweli wahitaji kipato endelevu, jali na tunza pia kifaa cha kazi.

SIMANZI ZAMBIA

Ni juzi tu wamesherehekea miaka 50 ya Uhuru wa nchi yao, ila jana Zambia imempoteza Rais wao Mhe. Sata huko London alipokuwa akipata matibabu. Habari zinasema Makamu wa Rais Mhe. Dk, Guy Scottambaye ni wa asili ya Kizungu ndio anashika madaraka mpaka uchaguzi utakapofanyika tena. RIP Rais wa Zambia.
Mhe. Dk. Guy Scott

UTANI MWINGINE WAHITAJI UJASIRI

Watoto wana namna nyingi za kufanya matani ila matani mengine yahitaji ujasiri mkubwa kuyakubali . Hapa huyu mtoto akiamua kufanya majaribio ya matumizi ya hilo panga, anafungua bucha. Tuwafundishe watoto wetu matani mazuri na yafaayo katika kujijenga binafsi na jamii. Ila pia tuwakumbushe matani mengine ambayo yanaweza kuleta madhara.

HUU NAO NI UBUNIFU

UBUNIFU

Katika kuboresha maisha na kuleta mvuto zaidi kimazingira, ubunifu ni muhimu.
Ubunifu katika michezo

Tuesday, 28 October 2014

MISAADA ISIVYOTUMIKA VIZURI

Hivi kweli tuliomba msaada wa net kujikinga na malaria au kuzikinga mboga zetu na malaria au wanyama/ndefu/wadudu waharibifu?

YAWEZEKANA KWELI KWAMBA MADREVA WETU HAWAJUI KUSOMA AU NI DHARAU???

Monday, 27 October 2014

KUMEKUCHA TUKAWAJIBIKE

Tulikotoka ni mbali , pengine asubuhi hii ndo unapasha ugali moto ule uwahi majukumu yako kama ni shule au kazini. Yote maisha, twende tukawajibike.
Tukauze mitumba sasa Gulioni
Nawe Boda boda usijali, hii ni zaidi ya Mshkaki
Mavuno ya mshambani nayo